Vitu vilivyopo katikati ya miguu yako

faq legs

Uume wangu ni dhaifu na sina nguvu za kushikiriki ngono. Kuna chochote ninachoweza kutumia ili kushiriki ngono kwa muda mrefu?

Ni kawaida kukosa nguvu za kushiriki katika ngono wakati mwingine na kuwa na uume dhaifu. Kuna mambo mengi yanayoathiri nguvu za kiume kwenye ngono kama afya zao za akili, lishe, na afya ya kimwili kwa ujumla. Magonjwa kama unyogovu, ugonjwa wa kisukari, na shinikizo la damu yanaweza kuathiri nguvu za kiume kwenye kushiriki ngono. Chaguo lako bora ni kumuuliza mtaalamu wa huduma za afya na kupata maoni yao.

Unaweza pia kumuona daktari ili kuona kama una ugonjwa wa kukosa nguvu za uume na kuna baadhi ya dawa ambazo unaweza pia kuchukua. Ikiwa unakabiliwa na aina fulani ya kukosa nguvu za kiume isiyohusiana na suala jingine, kuna baadhi ya dawa ambazo unaweza kuchukua.

Ninataka kutahiriwa lakini nina VVU, kuna tatizo?

Bila shaka unaweza kutahiriwa hata kama una VVU! Wanaume wengine wanadhani kuwa kutahiriwa ni kwa watu wasiokuwa na VVU ili kupunguza hatari ya kuambukizwa lakini kuna sababu nyingi (za jadi na za matibabu) kwamba kutahiriwa kunaweza kuwa sawa kwako pia. Ikiwa utatahiriwa, itakuwa ni wazo nzuri kuwa kwenye ARVs kwanza ili kuboresha mfumo wako wa kinga na kuhakikisha mchakato wa uponyaji unafanyika vizuri.

Wakati wote ninapofanya ngono na mpenzi wangu huwa namaliza haraka. Ni aibu. Nifanye nini?

Hii ni hali ya kawaida na inajulikana kama kumwaga mapema. Ni kawaida sana kwa vijana wadogo na hasa hupotea bila matibabu yoyote. Kuna mambo machache ambayo yanaweza kusaidia kupunguza kasi ya kumwaga kwako. Kwanza, anza taratibu. Pumzika kama unafikiri unapata msisimko haraka sana. Wanaume wengine hutumia kinga ili kupunguza msisimko kwenye uume wao ili kuzuia kumwaga haraka lakini kumbuka hutakiwi kutumia kinga zaidi ya moja kwa sababu zinaweza kupasuka. Ikiwa bado una mashaka, ongea na mtaalamu wa huduma za afya ambaye anaweza kutoa msaada wa ziada.

Wakati mwingine mimi hufanywa kwa ngono ya mkundu na inaumiza sana. Kuna chochote ninachoweza kufanya ili niifurahie zaidi?

Ngono ya mkundu haipaswi kuwa na maumivu. Mkundu wako umezungukwa na misuli ambayo ina asili ya kubana tofauti na uke, mkundu hauna kawaida ya kujilowesha wenyewe kwa hivyo ni mkavu sana. Ili kufanya ngono ya mkundu iweze kupendeza, unahitaji kuhakikisha kuwa mkundu wako umelainishwa na mafuta-maji. Tumia mafuta-maji kabla ya kujamiiana na wakati unapokauka. Ifuatayo, hakikisha misuli yako kuzunguka mkundu wako imetuliwa. Unaweza kutumia vidole vyako ili kupanua polepole misuli hii mpaka utakapohisi vizuri. Unapaswa pia kudhibiti jinsi ya kasi na kina unavyopenyaza ili uweze kutuliza polepole misuli yako. Ni rahisi kufanya hivyo ikiwa uko juu ili uweze kudhibiti jinsi mambo yanavyoenda.

Magonjwa ya zinaa

faq sti

Nimegundua kwamba mtu ninayejamiiana naye ana magonjwa ya zinaa. Nifanye nini?

Ni rahisi kwa magonjwa mengi ya zinaa kuambukizwa kati ya washirika wa ngono hata wakati kinga na mafuta-maji kutumiwa. Kwa hiyo ikiwa mtu uliyefanya nae ngono ana magonjwa ya zinaa unapaswa kwenda zahanati na umjulishe mhudumu wa huduma za afya. Kumbuka, wakati mwingine magonjwa ya zinaa hayana dalili hata kama umeambukizwa. Hivyo ni vyema kupima na kutibiwa.

Nawezaje kupimwa magonjwa ya zinaa?

Jinsi ya kupimwa kwa magonjwa ya zinaa itategemea aina gani za huduma za afya unazopata. Unaweza kupata huduma za afya za kirafiki kwa kuwasiliana na mashirika ya mitaa yako. Vituo vingi vya huduma za afya vitaweza kutumia tone dogo la damu yako ili kupima VVU na Sirifi. Baadhi ya zahanati huenda zisiweze kupima magonjwa ya zinaa kwa urahisi kama  Hepatitis A, B, na C, lakini bado unapaswa kuzungumza na mhudumu wa afya kuhusu magonjwa hayo. Hatimaye, magonjwa mengine ya zinaa kama Herpes, Chlamydia na Gono yanaweza kuchunguzwa au unaweza kupata tiba hata kama huna dalili ikiwa mpenzi wako ameambukizwa.

Ni maambukizi gani ambayo yanaweza kupata kama nimejamiiana na mtu mwingine bila kinga?

Unaweza kuambukizwa magonjwa ya zinaa kama hutumii kinga wakati wa kujamiiana na mwanaume mwingine au wanawake. Haya ni pamoja na Chlamydia na / au Gono, Syphilis, Hepatitis A, B, C, Vidonda (HPV), Herpes (HSV), na VVU. Pata maelezo zaidi kuhusu magonjwa ya zinaa haya hapa.

Kuna tatizo kwenye mkundu wangu, nadhani labda nina vidonda. Nifanyeje?

Vidonda vya mkunduni  husababishwa na virusi vya zinaa vinayoitwa virusi vya papilloma vya binadamu. Wahudumu wa afya wanaweza kutibu vidonda hivi kwa njia mbalimbali kulingana na matibabu (kuvipoza (kinajulikana kama cryotherapy), kwa kutumia creams au lotions au wakati mwingine kwa upasuaji. Baadhi ya wanaume hawapendi kuzungumzia hili na wahudumu ya afya au kuwajulisha kwamba wamejamiiwa kupitia ngono ya mkundu. Kama ni hivyo, unapaswa kuzungumza na mashirika ya mtaani kwako kupata wahudumu wa afya ambayo hutoa huduma nzuri na ya kirafiki kwa wanaume wanaojamiiana na wanaume.