header image

Wanaume na Ngono

Ngono: nini wanaume wanapaswa kujua

Ngono ni sehemu nzuri ya maisha yetu. Wanaume wanaweza kufanya ngono na washirika mbalimbali, au moja tu. Wanaume pia wanaweza kufurahia ngono kwa njia nyingi tofauti. Yote ni sawa.

Wajibu wa ngono ni kufanya maamuzi sahihi kwetu sisi wenyewe na washirika wetu kwa kuheshimiana, mawasiliano ya wazi na uaminifu. Hii inamaanisha kuangalia afya zetu na afya za washirika wetu.

Wanaume wanajamiiana na nani

Baadhi yetu tupo katika mahusiano au kwenye ndoa; wengine wetu hatujaoa. Baadhi yetu tuna washirika kadhaa wa ngono. Wanaume wengi wanafanya ngono na wanawake, wakati wengi wetu wanafanya ngono na wanaume na wanawake. Wengine hufanya ngono na wanaume tu.

Hatuwezi kuchagua kama tunavutiwa na wanawake, wanaume, au kwa jinsia zote; hii sio kitu tunaweza kuamua. Ni jinsi tulivyo.

Tunachagua wanaume au wanawake wangapi wa kufanya nao ngono na tunafanya uamuzi binafsi wa kufanya ngono tu na watu wazima wenzetu.

Wanaume wanafanya ngono ipi

men whatThere are many different kinds of sex.

Kuna aina nyingi za ngono.

Kumbusu, ngono ya mdomo (kulamba), ngono ya mkundu, ngono ya uke, ngono ya mapaja, ngono ya kikundi na ngono ya kuamua kutomasa tunaweza kuchagua kufanya na washirika wetu.

Baadhi ya vitendo hivi ni hatari kwa kupata VVU kuliko vingine. Kwa mfano, ngono ya mkundu bila kinga na mafuta-maji ya kulainisha ina hatari kubwa ya kupata VVU au kumuambukiza mwingine.

Wakati gani wanaume wanafanya ngono

Tunaweza kufanya ngono wakati nafsi zetu zinaturidhisha, au tunaweza kufanya ngono wakati tumekwisha kunywa au kutumia madawa ya kulevya na tunaweza kushindwa kufanya maamuzi sahihi. Ikiwa tunadhani tutafanya ngono ya mkundu au ya uke tunapaswa kuhakikisha kuwa tunatumia kinga na mafuta-maji ya kulainisha.